Simba Sc imeunguruma huko Uturuki ikiibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Batman AS katika mchezo wa Kimataifa wa kirafiki
Huo ulikuwa mchezo wa kuhitimisha pre-season ya takribani wiki tatu ambayo Simba waliweka huko Uturuki
Mabao ya Simba yalifungwa na Willy Onana, Saido Ntibazonkiza, Mohammed Hussein 'Zimbwe Jr' na John Bocco
Bocco na Kibu Denis wamekuwa na pre-season nzuri kila mmoja akipachika mabao mawili
Kibu alitoa pasi ya bao lililofungwa na Bocco wakati Ntibazonkiza, Fabrice Ngoma na Shomari Kapombe pia wakitia pasi za mabao mengine





