Baada ya kibegi cha Simba kupanda juu ya mlima Kilimanjaro ambako uzinduzi wa jezi ya Simba 2023/24 ulishuhudiwa, kibegi hicho sasa kinakwenda kupigwa mnada ambapo fedha zitakazopatikana zitakwenda kusaidia wodi za Mama na Mtoto kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Hospitali ya Zanzibar
Simba imetangaza kuwa Mnada huo utafanyika leo saa 2 usiku na utakuwa mbashara kupitia Azam TV
"Leo Jumatatu saa 2:00 usiku kupitia Azam TV tutafanya mnada maalum wa Kibegi pamoja na Jezi zilizopelekwa kileleni mwa Mlima Kilimanjaro kwa ajili ya uzinduzi wa jezi za msimu 2023/24. Pesa zitakazopatikana kwenye mnada huo zitatumika kuchangia ujenzi wa wodi za Mama na Mtoto kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Hospitali ya Zanzibar," ilisema taarifa ya Simba




