Mshambuliaji Sadio Mane anatarajia kufanyiwa vipimo vya afya leo kabla ya kusaini mkataba wa kuitumikia klabu ya Al-Nassr akitokea Bayern Munchen
Kwa mujibu wa mtandao wa Sky Sport, Mane atakamilisha uhamisho wake kwa dau la pauni milioni £24m
Mane ataungana na mshambuliaji Cristiano Ronaldo ambaye pia anaitumikia timu hiyo
Mane amekuwa na wakati mgumu tangu aliposajiliwa na Bayern Munich msimu uliopita
Tangu aingie kwenye mgogoro na mchezaji mwenzake wa Bayern Leroy Sane, mabosi wa Bayern walimuondoa katika mipango ya timu hiyo