Simba - Local

Chama awakaribisha Power Dynamos

Joel JJ By Joel JJ
β€’
3 Aug 2023
Chama awakaribisha Power Dynamos

Kiungo fundi wa Simba Clatous Chama amesema mabingwa wa Zambia, Power Dynamos watawapa mechi nzuri katika Simba Day Jumapili, August 06 katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Chama aliyewahi kuitumikia Power Dynamos kwa miezi sita kabla ya kusajiliwa na Simba msimu wa 2018/19, amesema Power Dynamos ni moja ya timu bora na zenye historia kubwa nchini Zambia

"Power Dynamos ni timu kubwa sana Zambia, wakati naanza kucheza mpira ligi kuu, msimu wa 2009/10, ndoto yangu kubwa ilikuwa kuichezea Power Dynamos, nashukuru nilicheza kwa muda mfupi kabla ya kusajiliwa na Simba"

"Ni timu nzuri walipotea kwa misimu kadhaa lakini nafurahi kuona wamerejea tena wakishinda ubingwa wa Zambia. Natarajia utakuwa mchezo mzuri kwa timu zote"

"Mimi nawaombea washinde mechi yao ya ligi ya mabingwa ili tukutane nao tena ili tuwapige..," alisema Chama

Simba na Power Dynamos zinaweza kukutana kwenye raundi ya kwanza ya ligi ya mabingwa barani Afrika kama Dynamos watashinda mchezo wa hatua ya awali dhidi ya African Star ya Namibia kwani mshindi wa mchezo huo atakutana na Simba inayoanzia raundi ya kwanza

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
9h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
10h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
10h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
13h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
17h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
17h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
18h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
19h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
19h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
20h ago
READ MORE β†’