Kikosi cha Yanga leo kimecheza mechi mbili za kirafiki katika uwanja wake wa mazoezi Avic Town
Asubuhi Yanga iliumana na Friends Rangers na kuibuka na ushindi wa mabao 6-1
Yanga imehitimisha mchezo wa pili jioni hii kwa kuumana na JKU ya Zanzibar mchezo uliomalizika kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana
Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi aliomba mechi hizo kuwapima wachezaji wake wote
Yanga imehitimisha pre-season na sasa inasubiri kuelekea mkoani Tanga kuikabili Azam Fc katika mchezo wa Ngao ya Jamii



