Tetesi za soka Ulaya, Jumamosi August 05 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th August 2023


Tetesi za soka Ulaya, Jumamosi August 05 2023

Barcelona watamfanya kiungo wa Manchester City, Bernardo Silva, 28, kuwa kipaumbele chao huku winga wa Ufaransa Ousmane Dembele, 26, akitarajiwa kujiunga na Paris St-Germain. (Mundo Deportivo - kwa Kihispania)

Kazi ya kocha wa West Ham David Moyes iko hatarini huku mvutano ukiongezeka katika klabu hiyo kuhusu malengo yao ya uhamisho. (Mail)

West Ham iko tayari kujadili mkataba wa kiungo wa Mexico Edson Alvarez na Ajax, baada ya kukubaliana masuala ya kibinafsi na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25. (Fabrizio Romano)

Meneja wa Manchester United Erik ten Hag anataka klabu hiyo kumnunua kiungo wa kati wa Real Madrid Mfaransa Aurelien Tchouameni, 23, ambaye pia analengwa na klabu ya Ujerumani Bayern Munich. (Sport - kwa Kihispania)

Kiungo wa Morocco Sofyan Amrabat ameachwa nje ya kikosi cha Fiorentina kwa ajili ya mechi za kirafiki za kujiandaa kwa msimu ujao wikendi hii huku Manchester United wakionyesha nia ya kutaka kumnunua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 . (Manchester Evening News)

Real Madrid wanatazamiwa kumenyana na Chelsea katika kinyang'anyiro cha kumsajili mshambuliaji wa Juventus na Serbia Dusan Vlahovic mwenye umri wa miaka 23 endapo juhudi zao za kumleta mshambuliaji wa PSG na Ufaransa Kylian Mbappe, 24, Bernabeu yatagongwa mwamba. (Cadenaser - kwa Kihispania)

Chelsea wanamfuatilia kiungo wa PSG na Argentina Leandro Parades, 29, baada ya kuchanganyikiwa katika jitihada zao za kumsajili mchezaji wa Brighton na Ecuador Moises Caicedo, 21. (Standard)

Manchester City wamempa kandarasi mpya mlinzi wa Uingereza Kyle Walker kwa nia ya kumbakisha mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 katika klabu hiyo huku Bayern Munich wakionyesha nia ya kutaka kumnunua . (Athletic - Usajili unahitajika)

Inter Milan wamekubali ofa ya Bayern Munich kwa ajili ya mlinda mlango wa Uswizi Yann Sommer na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34 atafanyiwa vipimo vya matibabu wiki ijayo kabla ya kusaini mkataba wa miaka miwili na klabu hiyo ya Italia. (Football Italia)

Atalanta iko tayari kuipiku Inter Milan katika mbio za kumsajili mshambuliaji wa West Ham na Italia Gianluca Scamacca, 24. (Football Italia)

Barcelona wako tayari kukubali ofa ya takriban euro milioni 10 (£8.6m) kumpata beki wa Marekani Sergino Dest, 22. (Athletic - Usajili unahitajika)

Chelsea wamewasiliana na wawekezaji kuhusu kuongeza mtaji wa $500m (£392m) kwa klabu hiyo na pesa zozote zitakazoingizwa kwa The Blues zinaweza kuwa kama malipo ya dau la klabu hiyo ya London. (Bloomberg - usajili unahitajika)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.