Azam Fc yaichapa Bandari Fc 2-0

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th August 2023


Azam Fc yaichapa Bandari Fc 2-0

Azam Fc imehitimisha maandalizi ya msimu mpya kibabe kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Bandari Fc ya Kenya katika mchezo wa Kimataifa wa kitafiki uliopigwa uwanja wa Azam Complex, Chamazi

Mabao ya Azam Fc yalifungwa na Sidibe na Prince Dube kiungo Feisal Salum 'Fei Toto' akitoa pasi ya bao la pili lililofungwa na Dube

Huo ulikuwa mchezo wa mwisho kwa Azam Fc katika maandalizi yake ya msimu mpya ambayo yalianzia Tunisia

Azam Fc sasa inaelekea mkoani Tanga kushiriki Ngao ya Jamii ikitarajiwa kuchuana na Yanga siku ya Jumatano


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.