Azam Fc imehitimisha maandalizi ya msimu mpya kibabe kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Bandari Fc ya Kenya katika mchezo wa Kimataifa wa kitafiki uliopigwa uwanja wa Azam Complex, Chamazi
Mabao ya Azam Fc yalifungwa na Sidibe na Prince Dube kiungo Feisal Salum 'Fei Toto' akitoa pasi ya bao la pili lililofungwa na Dube
Huo ulikuwa mchezo wa mwisho kwa Azam Fc katika maandalizi yake ya msimu mpya ambayo yalianzia Tunisia
Azam Fc sasa inaelekea mkoani Tanga kushiriki Ngao ya Jamii ikitarajiwa kuchuana na Yanga siku ya Jumatano



