Kikosi cha Singida Fountain Gate ambacho kipo tayari mkoani Tanga kwa ajili ya kucheza mechi za kusaka mshindi wa Ngao ya Jamii 2023/24, leo saa 1:00 usiku kitacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Coastal Union inayonolewa na kocha Mwinyi Zahera katika Uwanja wa Mkwakwani
Singida FG itacheza dhidi ya Simba SC Agosti 10 mechi ya kwanza kisha mshindi atacheza na mshindi wa mechi ya Yanga vs Azam inayopigwa Jumatano Agosti 9
Coastal Union inayonolewa na Kocha Mwinyi Zahera inajiandaa na msimu mpya unaotarajia kuanza wiki ijayo wakati Singida FG wako mkoani Tanga kwa takribani siku tatu wakijiandaa na mechi ya nusu fainali Ngao ya Jamii
Wapinzani wao Simba jana walikamilisha Tamasha la Simba Day kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Power Dynamos na wanatarajia kutua jijini Tanga siku ya Jumanne



