Yanga - Local

Documentary ya Yanga yafana

Joel JJ By Joel JJ
β€’
8 Aug 2023
Documentary ya Yanga yafana

Klabu ya Yanga jana ilizindua Documentary kwa ajili ya kumulika mafanikio waliyopata msimu uliopita katika mashindano mbalimbali

Katika msimu wa 20222/23, Yanga ilifanikiwa kushinda mataji yote ya ndani pamoja na kutinga fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika

Documentary hiyo inamulika kwa kina hatua kwa hatua yale yaliyokuwa yakijiri nyuma ya camera

Katika uzinduzi huo, Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe alisema wametengeza Documentary hiyo ili kuhifadhi katika kumbukumbu mafanikio ambayo walipata msimu uliopita hasa kucheza fainali ya kombe la Shirikisho la CAF

"Msimu uliopita tulipata mafanikio makubwa, kushinda mataji yote ya ndani na kucheza fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Ilikuwa mara ya kwanza kwa Yanga kufikia hatua hii naamini tulikuwa na kila sababu ya kuandaa Documentary hii ili kuhifadhi kumbukumbu hii kwa ajili ya vizazi vijavyo"

"Lakini pia Documentary hii imetoa nafasi kwa wengine kujifunza na kuona vile ambavyo tulipita milima na mabonde kuweza kufanikiwa kile tulichokipata"

"Sio nyakati zote zilikuwa za furaha, zipo nyakati ngumu ambazo tulipita, mashabiki wetu watapata kufahamu wakati mwingine ni kwa kiasi gani mambo sio rahisi kama yanavyoonekana nje," alisema Kamwe

Documentary hiyo itaonyeshwa na Azam Media kupitia Azam Max App kwa gharama ya Tsh 2,500/-

More Stories

Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
32m ago
READ MORE β†’
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
10h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
11h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
11h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
14h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
18h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
18h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
19h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
20h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
20h ago
READ MORE β†’