Nyota wa Paris Saint-Germain, Neymar, anataka kujiunga tena na Barcelona msimu huu wa majira ya joto, lakini kuna mjadala wa ndani katika klabu kuhusu usajili wa mshambuliaji huyo
Hata hivyo huenda isiwe rahisi kwa Neymar kurejea kunako klabu hiyo baada ya kocha wa Barcelona Xavi Hernandez kuonyesha kutomuhitaji
Kwa mujibu wa ESPN, Neymar mwenye umri wa miaka 31, angefurahi kujiunga tena na Barcelona, na vyanzo viliongeza kwamba kwa mara nyingine ameongeza uwezekano huo katika siku za hivi karibuni.
Uwezekano wa kuhama ni mdogo, hata hivyo, kwa sababu ya matatizo ya kifedha ya klabu na upinzani wa Xavi kurejea kwake.
Zikiwa zimesalia siku nne tu Barca waanze msimu wao wa ligi wa 2023-24, wameshindwa kusajili wachezaji wao wapya - Ilkay Gundogan, Oriol Romeu na Inigo Martinez - au wachezaji ambao wameongeza mikataba yao hivi karibuni.
Wana wachezaji 13 pekee wanaopatikana kwa mchezo wa Jumapili dhidi ya Getafe. Idadi hiyo inaweza kupunguzwa hadi 11 katika siku zijazo, huku Barca wakitarajia kukamilisha kuondoka kwa Franck Kessie kwenda Saudi Arabia na Ousmane Dembele kwenda PSG.
Klabu hiyo inafanya kazi kwa haraka kutatua tatizo hilo, na ujio wa Neymar utafanya hali kuwa ngumu zaidi, licha ya nia ya mchezaji huyo kuafikiana ili kufanikisha uhamisho huo.



