Bayern yamnasa Kane

Joel JJ By Joel JJ β€’ 11th August 2023


Bayern yamnasa Kane

Hatimaye klabu ya Bayern Munich imefanikiwa kumnasa mshambuliaji wa Tottenham Hotspurs Harry Kane ambaye pia ni nahodha wa timu ya Taifa ya Uingereza

Kane amesafiri kwenda Ujerumani kukamilisha vipimo vya afya kabla ya kutangazwa rasmi kuwa mchezaji wa Bayern

Bayern wamefikia makubaliano ya ada ya uhamisho pauni Milioni 120, ambapo Bayern watatanguliza pauni milioni 100

Kane ameitumikia Spurs kwa takribani miaka 10 akifunga mabao 280 katika mechi 435

Anaondoka akiwa mfungaji bora wa muda wote wa Tottenham Hotspurs


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.