Hatimaye klabu ya Bayern Munich imefanikiwa kumnasa mshambuliaji wa Tottenham Hotspurs Harry Kane ambaye pia ni nahodha wa timu ya Taifa ya Uingereza
Kane amesafiri kwenda Ujerumani kukamilisha vipimo vya afya kabla ya kutangazwa rasmi kuwa mchezaji wa Bayern
Bayern wamefikia makubaliano ya ada ya uhamisho pauni Milioni 120, ambapo Bayern watatanguliza pauni milioni 100
Kane ameitumikia Spurs kwa takribani miaka 10 akifunga mabao 280 katika mechi 435
Anaondoka akiwa mfungaji bora wa muda wote wa Tottenham Hotspurs



