Winga wa Yanga Skudu Makudubela jana alirejea uwanjani akifanya mazoezi mepesi siku moja baada ya kupata majeraha katika mchezo wa nusu fainali Ngao ya Jamii dhidi ya Azam Fc siku ya Jumatano
Hii ni habari njema kwa Wananchi kwani huenda wakamshuhudia Waziri wao wa raha kwenye mchezo wa fainali dhidi ya Simba siku ya Jumapili
Kikosi cha Yanga kiliendelea na mazoezi jana kujiandaa na mtanange huo wa fainali dhidi ya watani zao Simba ambao jana walishinda kwa mikwaju ya penati dhidi ya Singida FG baada ya matokeo ya suluhu ya bila kufungana
Yanga ilimsajili Skudu kutoka klabu ya Marumo Gallants ya Afrika Kusini akikabidhiwa jezi namba 6 ambayo ilipewa thamani kabla ya ujio wake
Mashabiki wa Yanga bado hawajashuhudia makali ya winga huyo mwenye uwezo mkubwa wa kuchezea mpira baada ya kucheza kwa dakika 7 tu mchezo dhidi ya Azam Fc na kuumia
Pengine wataipata nafasi hiyo siku ya jumapili katika mchezo dhidi ya watani zao Simba