Manchester City imeendeleza ilipoishia msimu uliopita walipata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Burnley katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu ya Uingereza
Ilkuwa mechi ya kwanza kwenye ligi kwa Kocha wa Burnley Vincent Kompany dhidi ya waajiri wake wa zamani Manchester City
Kompany aliitumikia Manchester City kwa miaka 10 akiwa nahodha wa timu hiyo kabla ya kustaafu misimu miwili iliyopita na kuhamia kwenye ukufunzi wa soka
Alifanikiwa kuirejesha Burnley ligi kuu msimu uliopita hata hivyo amekaribishwa kwenye ligi hiyo na kipigo cha kikatili katika uwanja wa nyumbani
Mabao mawili ya kipindi cha kwanza kutoka kwa Erling Haaland na juhudi za kipindi cha pili kutoka kwa Rodri yalitosha kupata ushindi huo dhidi ya wachezaji kumi wa Clarets, ambao walimshuhudia Anass Zaroury akitolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kumfanyia madhambi Kyle Walker.



