Simba - Local

Robertinho aipania Yanga, Ngao ya Jamii

Joel JJ By Joel JJ
12 Aug 2023
Robertinho aipania Yanga, Ngao ya Jamii

Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa fainali Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga ambao utapigwa kesho Jumapili katika uwanja wa Mkwakwani

Robertinho amesema hakuna kitakachobadilika katika mbinu zake, watashambulia lango la wapinzani wao na kuhakikisha wanakuwa imara bila ya mpira

"Mimi sio kocha wa kuficha mbinu, malengo yangu ni kuona tunacheza zaidi katika lango la wapinzani na kuwa imara tunapokuwa hatuna mpira"

"Tunafahamu tunakwenda kucheza na timu tofauti na ile tuliyokutana nayo msimu uliopita, wana wachezaji wapya na benchi la ufundi, tumeweka mkakati mzuri wa kuhakikisha tunashinda"

"Nafurahi tuna kikosi imara, wachezaji wote wako tayari lakini tutawatumia wale ambao wako katika kiwango bora zaidi kwa wakati huu," alisema Robertinho

Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake, beki Israel Mwenda amesema maandalizi ya mchezo huo yamekamilika na wachezaji wote wako tayari kwa mchezo

"Maandalizi yamekamilika na wachezaji wote tuko tayari kwa mchezo, kila mmoja anafahamu umuhimu wa mchezo," alisema

Baada ya kuikosa Ngao ya Jamii kwa misimu miwili mfululizo mbele ya Yanga, msimu huu Simba imejipanga kushinda ngao hiyo katika uwanja wa Mkwakwani

More Stories

Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa uhuru
27m ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
30m ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
47m ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
50m ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
1h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
2h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
13h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
13h ago
READ MORE →
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
13h ago
READ MORE →
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
17h ago
READ MORE →