Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa fainali Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga ambao utapigwa kesho Jumapili katika uwanja wa Mkwakwani
Robertinho amesema hakuna kitakachobadilika katika mbinu zake, watashambulia lango la wapinzani wao na kuhakikisha wanakuwa imara bila ya mpira
"Mimi sio kocha wa kuficha mbinu, malengo yangu ni kuona tunacheza zaidi katika lango la wapinzani na kuwa imara tunapokuwa hatuna mpira"
"Tunafahamu tunakwenda kucheza na timu tofauti na ile tuliyokutana nayo msimu uliopita, wana wachezaji wapya na benchi la ufundi, tumeweka mkakati mzuri wa kuhakikisha tunashinda"
"Nafurahi tuna kikosi imara, wachezaji wote wako tayari lakini tutawatumia wale ambao wako katika kiwango bora zaidi kwa wakati huu," alisema Robertinho
Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake, beki Israel Mwenda amesema maandalizi ya mchezo huo yamekamilika na wachezaji wote wako tayari kwa mchezo
"Maandalizi yamekamilika na wachezaji wote tuko tayari kwa mchezo, kila mmoja anafahamu umuhimu wa mchezo," alisema
Baada ya kuikosa Ngao ya Jamii kwa misimu miwili mfululizo mbele ya Yanga, msimu huu Simba imejipanga kushinda ngao hiyo katika uwanja wa Mkwakwani



