Simba yatambulisha kipa mpya

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th August 2023


Simba yatambulisha kipa mpya

Klabu ya Simba imetangaza kumsajili golikipa Ayoub Lakred raia wa Morocco kuja kuungana na Ally Salim, Charles Abel na Aishi Manula katika nafasi ya mlinda mlango

Lakred mwenye umri wa miaka 28, anakuja kuongeza nguvu kwenye kikosi cha Simba ambacho kina kibarua cha ligi ya ndani na ile ya kimataifa ikiwemo Africa Football League itakayoanza mwezi Oktoba

Mlinda lango huyo amewahi kuzitumikia AS FAR Rabat na RS berkane zote za Morocco


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.