Simba imefanikiwa kutwaa Ngao ya Jamii baada ya ushindi wa mikwaju 3-1 ya penati dhidi ya Yanga
Ulikuwa mchezo wa fainali ambao ulimalizika kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana baada ya dakika 90
Mlinda lango wa Simba Ally Salim alikuwa shujaa wa Simba akiokoa mikwaju mitatu ya penati katika mchezo ambao Simba haikuwa na dakika 90 bora
Baada ya kuikosa Ngao hiyo kwa misimu miwili, hatimaye mashabiki wa Simba leo wamefurahi kuishuhudia timu yao ikitwaa Ngao
Katika mchezo wa mapema kusaka mshindi wa tatu, Azam Fc iliichapa Singida FG mabao 2-0



