Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amewaomba radhi mashabiki wa timu hiyo baada ya kushindwa kutetea Ngao ya Jamii kwa msimu wa tatu mfululizo
Jana Yanga ilipoteza kwa mikwaju ya penati mchezo wa fainali dhidi ya Simba baada ya matokeo ya suluhu ya bila kufungana ndani ya dakika 90
Gamondi amesema walistahili kushinda mchezo huo kwani walicheza vizuri kuliko wapinzani wao lakini walikosa umakini katika eneo la umaliziaji
"Nawaomba radhi mashabiki kwa kupoteza mchezo huu kwenye penati, tulistahili kushinda. Kipindi cha kwanza tulicheza vizuri na kutengeneza nafasi lakini hatukuzitumia. Kipindi cha pili tulikuwa bora zaidi, sikumbuku kama wapinzani wetu walitengeneza nafasi yoyote ya wazi, hatukupata ushindi kwa sababu hatukufunga bao lakini tulicheza vizuri sana"
"Hili ni somo kwetu, tunarudi kwenye kiwanja cha mazoezi kufanyia kazi mapungufu hayo lakini kwa ujumla nimefurahishwa na jinsi wachezaji wamecheza katika dakika zote za mchezo," alisema Gamondi



