Beki kisiki wa Simba Hennock Inonga hatakuwa sehemu ya kikosi cha Simba kitakachoshuka dimbani kuzikabili Mtibwa Sugar na Dodoma Jiji zikiwa ni mechi za ligi kuu akiuguza majeraha ya bega
Kupitia taarifa iliyotolewa na Simba, Inonga anatarajiwa kuwa nje kwa wiki mbili akiuguza majeraha hayo ambayo alipata kwenye mchezo wa nusu fainali Ngao ya Jamii dhidi ya Singida FG
Inonga alikosa mchezo wa fainali dhidi ya Yanga nafasi yake ikichukuliwa na Kennedy Juma aliyeonyesha kiwango bora akishirikiana vyema na Che Fondoh Malone
Simba iko mkoani Morogoro ambapo siku ya Alhamisi itacheza mchezo wa kwanza wa ligi kuu msimu huu dhidi ya Mtibwa Sugar
Mchezo huo unatarajiwa kupigwa katika uwanja wa Manungu, Turiani



