Mtibwa Sugar yatamba kufanya vizuri msimu huu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 16th August 2023


Mtibwa Sugar yatamba kufanya vizuri msimu huu

Afisa Habari wa Mtibwa Sugar Thobias Kifaru amesema wamefanya maandalizi mazuri ya msimu mpya wakiwa tayari kufanya vizuri

Mtibwa Sugar itaanza msimu wa 2023/24 kwa kupambana na Simba SC, mechi itakayochezwa Agosti 17 katika uwanja wa Manungu

Kifaru amesema, wapo tayari kwa ajili ya msimu mpya na wana imani ya watafanya vizuri

"Tupo tayari kwa mechi zote ambazo tutacheza, hatuhofii ndio maana tupo kwenye ligi, sio Young Africans, Simba SC au Azam FC"

"Tunatambua lazima tucheze na timu zote, Wapinzani wetu tunawaheshimu nasi tunafanya maandalizi kupata matokeo mazuri"

"Makosa ambayo yalifanyika msimu wa 2022/23 benchi la ufundi limeyafanyia kazi," alisema Kifaru


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.