Azam Fc vs Kitayosce yavunjika

Joel JJ By Joel JJ β€’ 16th August 2023


Azam Fc vs Kitayosce yavunjika

Mchezo wa Ligi Kuu kati ya Azam Fc dhidi ya Kitayosce Fc umemalizwa dakika ya 19 baada ya wachezaji wa Kitayosce Fc kutokidhi taratibu za kinanuni kwa ajili ya mchezo huo kuendelea

Kitayosce waliingia uwanjani wakiwa na wachezaji nane na baadae wachezaji wao wawili wakaumia na hivyo kubaki sita uwanjani

Kanuni za FIFA haziruhusu mchezo kuendelea kama timu moja ina wachezaji pungufu ya saba uwanjani

Wakati mchezo huo unasitishwa Azam Fc walikuwa mbele kwa ushindi wa mabao 4-0, Feisal Salum akiwa mchezaji wa kwanza kufunga mabao matatu 'hat-trik' msimu huu

Bao la nne lilifungwa na Prince Dube


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.