Wekundu wa Msimbazi Simba Sc wameanza msimu wa ligi kuu 2023/24 kwa ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Mtibwa Sugar
Mabao ya Jean Baleke, Willy Onana na Fabrice Ngoma yaliipeleka Simba mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 3-2
Matheo Anthony alifunga mabao yote ya Mtibwa Sugar, kupitia nafasi mbili ambazo Mtibwa Sugar walipata kutokana na makosa ya safu ya ulinzi ya Simba
Simba ilirejea kipindi cha pili ikiendelea kutawala mchezo ambao kuingia kwa Saido Ntibazonkiza, Mzamiru Yassin na baadae Luis Miquissone kuliifanya Simba iendelee kumiliki mchezo
Bao la nne liliwekwa kambani na Clatous Chama aliyemalizika pasi murua kutoka kwa Luis Miquissone aliyeambaa na mpira upande wa kushoto kabla ya kujaza majaro iliyomkuta Chama katika nafasi nzuri na kuutumbukiza mpira kimiani