Mshambuliaji wa England, Theo Walcott ametangaza kustaafu soka akiwa na miaka 34
Walcott alianza kucheza Southampton mwaka 2005, mwaka 2006 alijiunga na Arsenal, mwaka 2018 alijiunga na Everton, 2021 akarejea Southampton
Amecheza michezo 563 na kufunga mabao 129 kwa ngazi ya klabu na michezo 47 na kufunga mabao manane akiwa na England
Majeraha ya mara kwa mara yamechangia kwa winga huyo mwenye kasi kutangaza kustaafu mapema



