Transfer - International

Tetesi za soka Ulaya, Jumamosi August 19 2023

Joel JJ By Joel JJ
19 Aug 2023
Tetesi za soka Ulaya, Jumamosi August 19 2023

Chelsea wana nia ya kumsajili mshambuliaji wa Marekani Folarin Balogun kutoka Arsenal, ambaye thamani yake ni £50m, huku Monaco pia wakimtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22, huku Inter Milan wakijitoa kwenye kinyang’anyiro cha kumsaka. ( Sky Sports)

Chelsea wanataka kumnunua beki wa kulia wa Real Valladolid na Uhispania Ivan Fresneda lakini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 18 anataka kuhamia Barcelona. (Mail)

Manchester City wana imani winga wa Ureno Bernardo Silva, 29, atasaini mkataba mpya licha ya uvumi kuhusu mustakabali wake msimu huu. (90 min)

The Blues pia wanakaribia kutoa kitita cha pauni milioni 11.8 kwa mlinda mlango wa Serbia na New England Revolution Djordje Petrovic, 23. (Evening Standard)

Fiorentina bado hawajapokea ofa rasmi kutoka kwa Manchester United kwa kiungo wa kati wa Morocco Sofyan Amrabat, 26. (Mirror)

Barcelona wapo kwenye mazungumzo ya kiwango cha juu na Manchester City ili kumsajili beki wa Ureno Joao Cancelo na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 anataka kuhama. ( Fabrizio Romano)

Luton wametuma ya maombi ya kutaka kujua kuhusu mkopo kwa mlinzi wa Tottenham Hotspur Muingereza Japhet Tanganga, 24 (Athletic - subscription required)

Mlinzi wa Manchester United na Ufaransa Raphael Varane, 30, anasakwa na klabu ya Saudi Arabia Al-Ittihad. ( Express)

Mshambulizi wa Barcelona Mhispania Ansu Fati, 20, amepewa ofa ya kwenda Paris St-Germain baada ya hapo awali kuhusishwa na Manchester United na Arsenal. (Sun)

Benjamin Pavard wa Bayern Munich , 27, anasalia kuwa mmoja wapo wa wachezaji wanaolengwa na Inter Milan huku beki huyo wa Ufaransa akiivutia pia Arsenal . (Evening Standard)

Mkufunzi wa West Ham David Moyes amedai kuwa kwa sasa hafikirii kumnunua kiungo wa kati wa Uingereza mwenye umri wa miaka 30 na nyota wa zamani wa Hammers Jesse Lingard. (Mail)

Southampton wana nia ya kumsajili kiungo wa kati wa Ujerumani Luca Kerber mwenye umri wa miaka 21 kutoka Saarbrucken. (Mail)

BBC

More Stories

Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa uhuru
53m ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
56m ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
1h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
1h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
1h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
3h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
13h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
13h ago
READ MORE →
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
14h ago
READ MORE →
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
17h ago
READ MORE →