Simba yaipania Dodoma Jiji Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 19th August 2023


Simba yaipania Dodoma Jiji Ligi Kuu

Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Dodoma Jiji ambao utapigwa kesho Jumapili katika uwanja wa Uhuru

Robertinho amesema wataingia katika mchezo huo kwa tahadhari lakini lengo ni kuhakikisha wanaondoka na alama zote tatu

"Tumekamilisha maandalizi kuelekea mchezo dhidi ya Dodoma Jiji, wachezaji wako katika hali nzuri kuelekea mchezo huu"

"Tunawaheshimu wapinzani wetu Dodoma Jiji lakini tutaingia uwanjani kwa lengo la kuhakikisha tunacheza soka safi na kushinda, " alisema Robertinho

Aidha Robertinho amebainisha kuwa wachezaji Hennock Inonga na Aubin Kramo wataendelea kukosekana wakiendelea kuuguza majeraha

Hennock anasumbuliwa na bega wakati Kramo ana tatizo la goti alilopata mazoezini kabla ya Ngao ya Jamii


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.