Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Dodoma Jiji ambao utapigwa kesho Jumapili katika uwanja wa Uhuru
Robertinho amesema wataingia katika mchezo huo kwa tahadhari lakini lengo ni kuhakikisha wanaondoka na alama zote tatu
"Tumekamilisha maandalizi kuelekea mchezo dhidi ya Dodoma Jiji, wachezaji wako katika hali nzuri kuelekea mchezo huu"
"Tunawaheshimu wapinzani wetu Dodoma Jiji lakini tutaingia uwanjani kwa lengo la kuhakikisha tunacheza soka safi na kushinda, " alisema Robertinho
Aidha Robertinho amebainisha kuwa wachezaji Hennock Inonga na Aubin Kramo wataendelea kukosekana wakiendelea kuuguza majeraha
Hennock anasumbuliwa na bega wakati Kramo ana tatizo la goti alilopata mazoezini kabla ya Ngao ya Jamii



