Manchester United imetangaza kuwa Mason Greenwood ataondoka katika klabu hiyo kufuatia uchunguzi wa ndani kuhusu madai ya jaribio la ubakaji, kudhibiti na mashitaka mengine yaliyokuwa yakimkabili
Baada ya Greenwood kufutiwa mashitaka yote, Manchester United ilitangaza kufanya uchunguzi maalum kabla ya kuamua hatma ya mchezaji huyo
"Manchester United imehitimisha uchunguzi wake wa ndani kuhusu tuhuma zilizotolewa dhidi ya Mason Greenwood"
"Wale wote waliohusika, ikiwa ni pamoja na Mason, wanatambua ugumu wa yeye kurejesha kazi yake katika Manchester United"
"Kwa hivyo imekubaliwa kuwa ingefaa zaidi kwake kufanya hivyo nje ya Old Trafford, na sasa tutashirikiana na Mason kufikia matokeo hayo," ilisema taarifa ya Manchester United