Mashabiki wa Simba wasitarajie kumshuhudia winga Peter Banda akiendelea kuwatumikia mabingwa hao wa Ngao ya Jamii
Simba inatarajiwa kumruhusu mchezaji huyo kwenda kusaka changamoto sehemu nyingine
Ni baada ya kukamilisha usajili wa mlinda lango Ayoub Lakred kutoka klabu ya FAR Rabbat ya Morocco
Simba inapaswa kuengua jina la mchezaji mmoja ili kusalia na wachezaji 12 ili kukidhi kanuni za shirikisho la mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Dirisha la usajili la ndani pamoja na lile la CAF yote yatafungwa August 31
Banda huenda akatimkia Ufaransa kuungana na Pape Ousmane Sakho ambaye Simba ilimuuza klabu ya Union Sportive Quevillaise-Rouen Metropol inayoshiriki ligi daraja la kwanza



