Msuva hana mpango wa kucheza Tanzania

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd August 2023


Msuva hana mpango wa kucheza Tanzania

Pamoja na kuhusishwa na klabu za Simba na Yanga, mshambuliaji wa timu ya Taifa 'Taifa Stars' Simon Msuva bado ana malengo ya kwenda kusakata kabumbu nje ya nchi

Mzee Happygod Msuva ambaye ni Baba mzazi na msimamizi wa mchezaji huyo, amesema kwa sasa mwanawe hafikirii kucheza Tanzania

"Mwanangu ananiambia, baba bado nataka kucheza nje ikitokea kucheza hapa nyumbani labda baadae lakini kwa sasa acha nikapammbane huko kwanza"

"Mambo yakikamilika tutaweka wazi lakini wanamichezo wajue sasa hivi Msuva kucheza hapa nyumbani hapana acha akapambane kama ambavyo anahitaji yeye," alisema Mzee Msuva

Msimu uliopita Msuva aliitumikia timu ya AL-QADSIAH inayoshiriki ligi daraja la pili huko Uarabuni. Alirejea nchini baada ya mkataba wake kumalizika

Mpaka sasa bado haijafahamika anaelekea wapi baada ya kukataa ofa za klabu za ndani


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.