Pamoja na kuhusishwa na klabu za Simba na Yanga, mshambuliaji wa timu ya Taifa 'Taifa Stars' Simon Msuva bado ana malengo ya kwenda kusakata kabumbu nje ya nchi
Mzee Happygod Msuva ambaye ni Baba mzazi na msimamizi wa mchezaji huyo, amesema kwa sasa mwanawe hafikirii kucheza Tanzania
"Mwanangu ananiambia, baba bado nataka kucheza nje ikitokea kucheza hapa nyumbani labda baadae lakini kwa sasa acha nikapammbane huko kwanza"
"Mambo yakikamilika tutaweka wazi lakini wanamichezo wajue sasa hivi Msuva kucheza hapa nyumbani hapana acha akapambane kama ambavyo anahitaji yeye," alisema Mzee Msuva
Msimu uliopita Msuva aliitumikia timu ya AL-QADSIAH inayoshiriki ligi daraja la pili huko Uarabuni. Alirejea nchini baada ya mkataba wake kumalizika
Mpaka sasa bado haijafahamika anaelekea wapi baada ya kukataa ofa za klabu za ndani



