Yanga vs KMC hapatoshi Azam Complex leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd August 2023


Yanga vs KMC hapatoshi Azam Complex leo

Ligi Kuu ya NBC inaendelea leo ambapo mchezo mmoja utapigwa uwanja wa Azam Complex, Chamazi jijini Dar es salaam

Mabingwa watetezi wa ligi hiyo Yanga watakuwa wenyeji wa KMC katika mchezo wa derby

Utakuwa mchezo wa kwanza kwa Yanga msimu huu 2023/24 wakati KMC watakuwa wakicheza mechi yao ya pili msimu huu

Walianzia Ruangwa ambako walilazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Namungo Fc

Ni mchezo unaotarajiwa kuwa na upinzani mkali, wenyeji Yanga wakipewa nafasi zaidi kutokana na ubora wa kikosi chao

Yanga imetoka kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Asas Fc katika mchezo wa mkondo wa kwanza hatua ya awali ligi ya mabingwa barani Afrika

Wakiwa mabingwa watetezi watataka kuanza vyema msimu ili kuwasogelea watani za Simba walio kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kushinda mechi zao zote mbili za kwanza

Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi kwa mara ya kwanza ataiongoza timu hiyo katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya KMC ambayo pia inaongozwa na Kocha mpya Abdihamid Moalin ambaye amewahi kuinoa klabu ya Azam Fc


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.