Simba - Yanga - Local

Simba vs Power Dynamos, Yanga vs El Merrikh Ligi ya Mabingwa Afrika

Joel JJ By Joel JJ
β€’
27 Aug 2023
Simba vs Power Dynamos, Yanga vs El Merrikh Ligi ya Mabingwa Afrika

Mabingwa wa Zambia Power Dynamos watachuana na Simba katika mchezo wa raundi ya kwanza ligi ya mabingwa barani Afrika

Ni baada ya Power Dynamos kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya African Stars jana na hivyo kufuzu raundi ya kwanza kwa faida ya bao la ugenini baada ya kuchapwa mabao 2-1 katika mchezo wa mkondo wa kwanza

Mchezo wa kwanza utapigwa Septemba 15 huko Zambia na mchezo wa marudiano kupigwa Septemba 29 jijini Dar es salaam

Simba na Power Dynamos zilichuana kwenye Tamasha la Simba Day, Wekundu wa Msimbazi wakiibuka na ushindi wa mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

Timu hizo zinakutana tena mara mbili kuwania tiketi ya kutinga hatua ya makundi

Wakati Simba ikichuana na Power Dynamos, Watani zao Yanga wao watachuana na El Merrikh ya Sudan

Jana Yanga ilitinga raundi ya kwanza kwa ushindi wa jumla wa mabao 7-1 dhidi ya Asas Fc ya Djibout wakati El Merrikh walifuzu kwa faida ya bao la ugenini baada ya matokeo ya suluhu ya bila kufungana dhidi ya Otoho ya Congo Brazaville

Simba na Yanga zote zitaanzia ugenini katika mechi za kwanza na kumalizia nyumbani mechi zao za marudiano

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’