Transfer - International

Tetesi za soka Ulaya, Jumatano August 30 2023

Joel JJ By Joel JJ
30 Aug 2023
Tetesi za soka Ulaya, Jumatano August 30 2023

Chelsea wanaweza kuwasilisha ofa ya kumnunua mshambuliaji wa Brentford na England aliyekadiriwa kuwa na thamani ya pauni milioni 80 Ivan Toney, 27, kabla ya dirisha la usajili kufungwa tarehe 1 Septemba. (Independent)

Tottenham imewapa Bayern Munich nafasi ya kumsajili beki wa Uingereza, Eric Dier, 29. (Sky Sports Germany - In Deutsch)

Manchester United wamewasiliana na Lyon kuhusu uhamisho wa mkopo kwa beki wao wa kushoto wa Argentina, Nicolas Tagliafico, 30. (Le Parisien - In French)

Besiktas wanatazamiwa kumpa mshambuliaji wa Manchester United Muingereza Mason Greenwood mwenye umri wa miaka 21 ofa ya kurejea kwenye soka baada ya kutangazwa kuwa ataondoka Old Trafford. (i sport)

Manchester United pia wamewasilisha pendekezo la kumsajili beki wa kushoto wa Uhispania Marc Cucurella, 25, kwa mkopo kutoka Chelsea. (Subscription Required)

Chelsea imepokea ripoti ya uchunguzi kutoka kwa Bayern Munich kuhusu kiungo wa kati wa Uingereza Conor Gallagher, 23, huku mlinzi wa Uingereza chini ya umri wa miaka 21 Trevoh Chalobah, 24, pia akiwa tayari kuhamia kwa mabingwa hao wa Bundesliga. (talkSPORT)

The Blues wanafikiria kuchukua hatua ya kumrejesha mshambuliaji wa Atletico Madrid na Ureno Joao Felix baada ya mchezaji huyo wa miaka 23 kucheza kwa mkopo Stamford Bridge msimu uliopita. (90 min)

Aston Villa wako kwenye mazungumzo na Barcelona kuhusu mpango wa kumnunua beki wa Ufaransa, Clement Lenglet, 28. (Fabrizio Romano)

Fulham wako kwenye mazungumzo ya kiwango cha juu na Everton ili kumsajili kiungo wao wa kati wa Nigeria Alex Iwobi, 27. (talkSPORT)

Fulham pia wamekubali mkataba na Sevilla kwa ajili ya kumnunua fowadi wa Argentina Lucas Ocampos, 29. (Telegraph - Subscription Required) Kuna uwezekano mkubwa kwamba West Ham watampa mchezaji huru na kiungo wa zamani wa Uingereza Jesse Lingard, 30, mkataba wa muda mfupi. (Standard)

Nottingham Forest wamekubali mkataba wa mkopo na Arsenal kwa ajili ya beki wao wa kushoto Mreno mwenye umri wa miaka 23 Nuno Tavares. (Fabrizio Romano)

Lakini Arsenal wamekataa mpango wa Chelsea kumnunua mshambuliaji wa Uingereza Emile Smith Rowe, 23. (Mail)

Wolves wanachunguza kumnunua mshambuliaji wa Club Libertad wa Paraguay, Enso Gonzalez, 18. (Football Insider)

West Ham wako kwenye mazungumzo na Paris St-Germain kuhusu kumsajili mshambuliaji wa Ufaransa, Hugo Ekitike, 21. (Sky Sports)

Crystal Palace pia wamewasilisha ofa ya mkopo kwa Ekitike. (L'Equipe - In French)

Luton wanataka kumnunua beki wa Arsenal mwenye umri wa miaka 27 kutoka Uingereza Rob Holding kwa mkopo. (Standard)

Beki wa Liverpool Muingereza Nat Phillips anaweza kuondoka kabla ya dirisha la uhamisho kukamilika, huku Middlesbrough ikiwa miongoni mwa vilabu vinavyotaka kumtoa kwa mkopo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26. (Subscription Required)

BBC

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
7h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
8h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
10h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
10h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
11h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
11h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
12h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
12h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
12h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
14h ago
READ MORE →