Jana viongozi wa klabu ya Simba walimtembelea Balozi wa Uturuki nchini, Dkt. Mehmet Gulluoglu kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushirikiano ambao ubalozi huo ulitoa wakati Simba ilipoweka kambi ya maandalizi ya msimu nchini Uturuki
Simba imedhamiria kujenga uhusiano endelevu baina yake na Serikali ya Uturuki kupitia Ubalozi wa nchi hiyo
Katika mazungumzo hayo Mwenyekiti wa Bodi ya Simba, Salim Abdallah alimshukuru Balozi wa kwa ushirikiano mkubwa walioonyesha na kuahidi kuendeleza ushirikiano mbalimbali na klabu ya Simba ikiwemo soka la vijana, timu ya wakubwa na timu ya wanawake
Kwa upande wake balozi wa Uturuki, Dr. Mehmet Gulluoglu alishukuru Klabu ya Simba kwa kuchagua Uturuki kama sehemu ya kuweka kambi yake kabla msimu kuanza na ameahidi kushirikiana na Simba katika maeneo mbalimbali
Kwenye ziara hiyo ya ubalozi wa Uturuki pia alikuwepo Mwenyekiti wa Simba Murtaza Mangugu, Mtendaji Mkuu wa Simba, Imani Kajula, Mkuu wa Oparesheni za Mpira, Mathew Shayo na Mkuu wa Utawala wa Klabu ya Simba, Belinda Paul




