Simba kushirikiana na ubalozi wa Uturuki

Joel JJ By Joel JJ β€’ 30th August 2023


Simba kushirikiana na ubalozi wa Uturuki

Jana viongozi wa klabu ya Simba walimtembelea Balozi wa Uturuki nchini, Dkt. Mehmet Gulluoglu kwa ajili ya kutoa shukrani kwa ushirikiano ambao ubalozi huo ulitoa wakati Simba ilipoweka kambi ya maandalizi ya msimu nchini Uturuki

Simba imedhamiria kujenga uhusiano endelevu baina yake na Serikali ya Uturuki kupitia Ubalozi wa nchi hiyo

Katika mazungumzo hayo Mwenyekiti wa Bodi ya Simba, Salim Abdallah alimshukuru Balozi wa kwa ushirikiano mkubwa walioonyesha na kuahidi kuendeleza ushirikiano mbalimbali na klabu ya Simba ikiwemo soka la vijana, timu ya wakubwa na timu ya wanawake

Kwa upande wake balozi wa Uturuki, Dr. Mehmet Gulluoglu alishukuru Klabu ya Simba kwa kuchagua Uturuki kama sehemu ya kuweka kambi yake kabla msimu kuanza na ameahidi kushirikiana na Simba katika maeneo mbalimbali

Kwenye ziara hiyo ya ubalozi wa Uturuki pia alikuwepo Mwenyekiti wa Simba Murtaza Mangugu, Mtendaji Mkuu wa Simba, Imani Kajula, Mkuu wa Oparesheni za Mpira, Mathew Shayo na Mkuu wa Utawala wa Klabu ya Simba, Belinda Paul


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.