Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) limeitaarifu klabu ya Yanga kuwa mchezo wa mkondo wa kwanza kuwania tiketi ya kutinga hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya El Merrikh utapigwa katika uwanja wa Pele nchini Rwanda
Mchezo huo umepangwa kupigwa Septemba 16 na mchezo wa marudiano kupigwa jijini Dar es salaam Septemba 29
Awali kulikuwa na taarifa kuwa El Merrikh waliomba kubadili uwanja kuupeleka mchezo huo nchini Morocco lakini ni wazi maombi hayo yamegonga mwamba
Ni rasmi sasa Septemba 16 mabingwa hao wa Tanzania Bara watakuwa Rwanda katika mchezo ambao bila shaka watapata uungwaji mkono mkubwa kutoka kwa Wananchi wa Rwanda
Yanga ina umaarufu mkubwa Rwanda kutokana na kuwahi kuwasajili wachezaji mahiri kutoka Rwanda akiwemo Haruna Niyonzima nahodha wa zamani wa timu ya Taifa ya Rwanda



