Dk Ndumbaro alishinda rufaa - TFF

Joel JJ By Joel JJ β€’ 2nd September 2023


Dk Ndumbaro alishinda rufaa - TFF

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa ufafanuzi kuhusiana na taarifa zinazoenea mitandaoni kuhusu kufungiwa kwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Damas Ndumbaro

Kupitia taarifa yake ya leo Septemba 2, 2023 TFF imebainisha kwamba usahihi ni kuwa Waziri Dk Ndumbaro alifungiwa miaka saba na uongozi uliopita wa TFF

Hata hivyo, hakukubaliana na uamuzi huo ambapo alikata rufani katika Kamati ya Rufani ya Nidhamu ya TFF kupinga adhabu hiyo

Hivyo, Kamati ya Rufani ya Nidhamu ya TFF chini ya uongozi wa sasa ilisikiliza rufani hiyo mwaka 2017 ambapo Waziri Dk Ndumbaro alishinda, hivyo kuondolewa adhabu ya kufungiwa

Kwa sasa Waziri Dk Ndumbaro ni Mwenyekiti wa Kamati ya Rufani ya Leseni za Klabu ya TEE


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.