Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa ufafanuzi kuhusiana na taarifa zinazoenea mitandaoni kuhusu kufungiwa kwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Damas Ndumbaro
Kupitia taarifa yake ya leo Septemba 2, 2023 TFF imebainisha kwamba usahihi ni kuwa Waziri Dk Ndumbaro alifungiwa miaka saba na uongozi uliopita wa TFF
Hata hivyo, hakukubaliana na uamuzi huo ambapo alikata rufani katika Kamati ya Rufani ya Nidhamu ya TFF kupinga adhabu hiyo
Hivyo, Kamati ya Rufani ya Nidhamu ya TFF chini ya uongozi wa sasa ilisikiliza rufani hiyo mwaka 2017 ambapo Waziri Dk Ndumbaro alishinda, hivyo kuondolewa adhabu ya kufungiwa
Kwa sasa Waziri Dk Ndumbaro ni Mwenyekiti wa Kamati ya Rufani ya Leseni za Klabu ya TEE



