Yanga - Local

Skudu kamili kuwapa furaha Wananchi

Joel JJ By Joel JJ
5 Sep 2023
Skudu kamili kuwapa furaha Wananchi

Kiungo mshambuliaji wa Yanga Skudu Makudubela amepona majeraha akiwa miongoni mwa wachezaji wanaojifua kwa ajili ya mchezo wa kuwania tiketi ya kutinga hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya El Merrikh

Kikosi cha Yanga kitasafiri Rwanda kuikabili El Merrikh katika mchezo wa mkondo wa kwanza utakaofanyika uwanja wa Pele, Septemba 16

Skudu alipata majeraha katika mchezo wa nusu fainali Ngao ya Jamii dhidi ya Azam Fc, akicheza kwa dakika saba tu katika mchezo ambao Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 2-0

Baadae hakuonekana tena uwanjani akiuguza majeraha hayo lakini sasa amepona na kurejea rasmi kikosini

Mashabiki wa Yanga tayari wameona ubora wa nyota wote waliosajiliwa isipokuwa Skudu tu, ambaye pengine wanaweza kumshuhudia nchini Rwanda

Kabla ya kupata majeraha Skudu alikuwa miongoni mwa wachezaji wa kikosi cha kwanza cha kocha Miguel Gamondi

Alitumika kwa dakika 45 katika mchezo wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya Kaizer Chiefs na pia kucheza mechi kadhaa za kirafiki Avic Town

Baada ya kuyaona makali ya Maxi Nzengeli na Pacome Zouzoua 'profesa', bila shaka ni zamu ya Skudu kuonyesha alichowaletea Wananchi

More Stories

SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
25m ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
2h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
12h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
12h ago
READ MORE →
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
13h ago
READ MORE →
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
16h ago
READ MORE →
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
20h ago
READ MORE →
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
20h ago
READ MORE →
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
21h ago
READ MORE →
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
21h ago
READ MORE →