Baada ya Mason Greenwood, nyota mwingine wa Manchester United amedaiwa kumshambulia mpenzi wake wa zamani alipokuwa mjamzito ikiwa ni pamoja na kumpiga kichwani na kumkata mkono hadi kwenye mfupa
Winga Antony Santos anachunguzwa na mahakama ya Mjini Sao Paulo huko Brazil kwa tuhuma za unyanyasaji wa nyumbani dhidi ya mpenzi wake wa zamani Gabriela Cavallin
Jarida la UOL la Brazil linaripoti kwamba imekuwa na ufikiaji wa picha, video, mazungumzo na ushuhuda kutoka kwa mashahidi ambao unaonyesha vitisho na mashambulizi ya kimwili kutoka kwa Antony
Moja ya video za uchunguzi huo inaonyesha jeraha lililofichua mifupa ya vidole vya Gabriela
Anthony amezikana tuhuma hizo huku akisubiri hatma ya uchunguzi wa Jeshi la Polisi Brazil
Mchezaji huyo ameenguliwa katika kikosi cha timu ya Taifa ya Brazil



