Simba yaichapa Cosmopolitan 5-1

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th September 2023


Simba yaichapa Cosmopolitan 5-1

Klabu ya Simba leo imecheza mechi ya kirafiki dhidi ya Cosmopolitan FC katika uwanja wake wa Mo Simba Arena uliopo Bunju nje kidogo ya jiji la Dar es saalam

Matokeo ya mchezo huo ni kuwa Simba imeibuka na ushindi wa mabao 5-1. Mabao ya Simba yalifungwa na Moses Phiri, Jean Baleke, Willy Onana, Aubin Kramo na Shaban Idd Chilunda

Huo ni mchezo wa pili wa kirafiki kwa Simba katika kipindi cha siku nne. Siku ya Jumamosi Simba iliichapa Kipanga Fc mabao 3-0 katika mchezo mwingine wa kirafiki yakiwa ni maandalizi kuelekea mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Power Dynamos


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.