Onditi arejea Azam Fc

Joel JJ By Joel JJ β€’ 6th September 2023


Onditi arejea Azam Fc

Klabu ya Azam Fc imemrejesha kiungo mkabaji Samwel Onditi aaliyekuwa akikipiga kwa mkopo Geita Gold

Benchi la ufundi la Azam Fc chini ya kocha Dabo, limependekeza kurejeshwa kwa kiungo huyo ili kuimarisha safu ya kiungo

Onditi anatarajiwa kusaini mkataba wa muda mrefu zaidi

Azam Fc imekuwa ikiandamwa sana na majeraha kwa wachezaji wao wanaotumikia eneo la kiungo

Walimsajili Yannick Bangala kutoka klabu ya Yanga lakini nyota huyo akaumia mara baada ya kujiunga nao

Licha ya kurejea kikosini bado hana utimamu wa kucheza dakika 90

Saospeter Bajana ni kiungo mwingine tegemeo ambaye pia alipata majeraha na kukosekana katika mechi ya mkondo wa pili kuwania kufuzu raundi ya kwanza ya CAF CC dhidi Fasil Kenema na Ethiopia Azam Fc ikitupwa nje kupitia mikwaju ya penati


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.