Kramo, Miquissone waongeza matumaini Simba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 6th September 2023


Kramo, Miquissone waongeza matumaini Simba

Kocha Mkuu wa Simba, Roberto Oliveira 'Robertinho' amesema ubora wa Luis Miquissone na Aubin Kramo unamuongezea upana wa kikosi kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa na African Football League

Akizungumza maendelea ya wachezaji hao baada ya kucheza mechi mbili za kirafiki, Robertinho amesema nyota hao wameendelea kuimarika na wanampa matumaini kuelekea mechi muhimu za ligi ya mabingwa na African Football League

"Nimewapa nafasi wachezaji wote ili kuona uwezo wa kila mmoja. Nafurahi kuona Miquissone ameanza kuonyesha uwezo mzuri, amecheza kwa dakika zote 90 na ameonyesha kiwango bora"

"Kwa upande wa Kramo licha ya kuingia kipindi cha pili kwenye mechi zote mbili za kirafiki, pia amenipa kitu kikubwa akifunga mabao mawili. Nitaendelea kumpa nafasi zaidi ili kuwa bora zaidi ya alipo sasa"

"Ni mchezaji mzuri lakini bado naendelea kumpa muda zaidi ili apate uzoefu wa ligi ya Tanzania. Tayari nimeanza kumpa dakika chache kwenye mechi za kirafiki na ameonyesha uwezo mkubwa kwani ni miongoni mwa wachezaji watakaocheza mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na naamini watatusaidia," alisema Robertinho

Simba inaendelea na mazoezi Mo Simba Arena kujiandaa na mchezo wa mkondo wa kwanza kuwania kufuzu hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Power Dynamo

Mchezo huo utapigwa Septemba 16 katika uwanja wa Levy Mwanawasa huko Zambia


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.