Tetesi za soka Ulaya, Ijumaa Septemba 08 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 8th September 2023


Tetesi za soka Ulaya, Ijumaa Septemba 08 2023

Winga wa Manchester United Jadon Sancho alikuwa akilengwa na Al-Ettifaq kabla ya dirisha la Ligi Kuu ya Saudia kufungwa Alhamisi walipokuwa wakijaribu kumsajili kwa mkopo mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza mwenye umri wa miaka 23. (CBS Sports)

Kocha wa zamani wa Brighton na Chelsea Graham Potter, 48, amekataa kuchukua nafasi ya Laurent Blanc katika klabu ya Lyon ya Ufaransa. (90 min)

Mshambuliaji wa zamani wa Uingereza Wayne Rooney, 37, anaweza kugombea Birmingham City ikiwa mkufunzi wa sasa John Eustace, ambaye amekuwa akihusishwa na Swansea na Rangers, ataondoka katika klabu hiyo. (Telegraph - usajili unahitajika)

Arsenal wanatumai kuwa wanaweza kufikia makubaliano ya uhamisho wa winga wa Ivory Coast Nicolas Pepe kuhamia Uturuki, huku Besiktas na Trabzonspor wakisemekana kumtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28. (Evening Standard)

Chelsea ilikuwa na ofa ya pauni milioni 23 kwa winga wa Norway Antonio Nusa iliyokataliwa na Club Brugge siku ya mwisho ya uhamisho na itakabiliwa na ushindani mkubwa wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 18 katika siku zijazo huku akitazamwa na angalau klabu zingine 20. (Evening Standard)

Kiungo mshambuliaji wa Uingereza Jesse Lingard, 30, alitazamiwa kuichezea West Ham katika mechi ya kirafiki ya bila mashabiki dhidi ya Ipswich, huku The Hammers wakifikiria kumpa mkataba mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United. (Mail)

Ajenti wa winga wa Napoli Kvicha Kvaratskhelia anasema mchezaji huyo wa kimataifa wa Georgia mwenye umri wa miaka 22 anaridhika katika kikosi cha Serie A na kwamba "hatukuwahi kuzungumza kuhusu kutaka kubadilisha klabu". (CalcioNapoli24, kupitia Football Italia)

Fulham wanajadiliana na kiungo wa kati wa Uingereza Harrison Reed kuhusu kandarasi mpya, huku Cottagers wakiwa wamekataa dau la pauni milioni 3 kutoka kwa Wolves kwa ajili ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 mwishoni mwa dirisha la uhamisho. (Evening Standard)

Bournemouth ilikataa dau la mwisho la pauni milioni 20 kwa mlinzi wa Uingereza Lloyd Kelly msimu wa joto na Tottenham Hotspur wanaweza kuunganishwa na Liverpool na Newcastle United kutaka kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 mwezi Januari. (90 min)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.