Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi ameibuka kuwa Kocha bora wa ligi kuu ya NBC kwa mwezi August 2023
Gamondi ameshinda tuzo hiyo ya kwanza msimu huu baada ya kuiongoza Yanga kupata ushindi katika mechi mbili za Ligi Kuu huku ikifunga mabao 10
Wakati Gamondi akishinda tuzo hiyo, kiungo mshambuliaji Maxi Nzengeli ameshinda tuzo ya mchezaji bora
Katika mwezi August, Maxi alifunga mabao mawili na kutoa pasi moja ya bao akihusika katika mabao matatu kati ya mabao 10 yaliyofungwa na Yanga

Tuzo ya Meneja bora imechukuliwa na Godfrey Komba ambaye ni Meneja wa Uwanja wa Manungu ulioko Turiani mkoani Morogoro



