Gamondi, Maxi washinda tuzo Ligi Kuu August

Joel JJ By Joel JJ β€’ 11th September 2023


Gamondi, Maxi washinda tuzo Ligi Kuu August

Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi ameibuka kuwa Kocha bora wa ligi kuu ya NBC kwa mwezi August 2023

Gamondi ameshinda tuzo hiyo ya kwanza msimu huu baada ya kuiongoza Yanga kupata ushindi katika mechi mbili za Ligi Kuu huku ikifunga mabao 10

Wakati Gamondi akishinda tuzo hiyo, kiungo mshambuliaji Maxi Nzengeli ameshinda tuzo ya mchezaji bora

Katika mwezi August, Maxi alifunga mabao mawili na kutoa pasi moja ya bao akihusika katika mabao matatu kati ya mabao 10 yaliyofungwa na Yanga

Tuzo ya Meneja bora imechukuliwa na Godfrey Komba ambaye ni Meneja wa Uwanja wa Manungu ulioko Turiani mkoani Morogoro


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.