Kikosi cha Yanga kitaondoka nchini leo kuelekea Rwanda wanakokabiliwa na mchezo wa kuwania kufuzu hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Al Merrikh
Mchezo huo utapigwa Jumamosi, Septemba 16 katika uwanja wa Pele, Kigali
Yanga leo itasafiri bila ya nahodha wake Bakari Nondo Mwamnyeto anayekabiliwa na matatizo ya kifamilia
Kulingana na taarifa iliyotolewa na Yanga, Kocha Mkuu wa timu hiyo Miguel Gamondi amemruhusu Mwamnyeto akashughulikie changamoto za kifamilia
Yanga inakwenda Rwanda ikiwa na kundi kubwa la mashabiki ambapo takribani mabasi 50 yaliondoka jana



