Yanga kuifuata Al Merrikh bila Mwamnyeto

Joel JJ By Joel JJ β€’ 14th September 2023


Yanga kuifuata Al Merrikh bila Mwamnyeto

Kikosi cha Yanga kitaondoka nchini leo kuelekea Rwanda wanakokabiliwa na mchezo wa kuwania kufuzu hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Al Merrikh

Mchezo huo utapigwa Jumamosi, Septemba 16 katika uwanja wa Pele, Kigali

Yanga leo itasafiri bila ya nahodha wake Bakari Nondo Mwamnyeto anayekabiliwa na matatizo ya kifamilia

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Yanga, Kocha Mkuu wa timu hiyo Miguel Gamondi amemruhusu Mwamnyeto akashughulikie changamoto za kifamilia

Yanga inakwenda Rwanda ikiwa na kundi kubwa la mashabiki ambapo takribani mabasi 50 yaliondoka jana


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.