USM Alger mabingwa CAF Super Cup

Joel JJ By Joel JJ β€’ 16th September 2023


USM Alger mabingwa CAF Super Cup

Klabu ya USM Alger kutoka Algeria jana ilifanikiwa kutwaa taji la CAF Super Cup baada ya kuichapa Al Ahly bao 1-0 katika mchezo uliopigwa Saudi Arabia

USM Alger ni mabingwa wa kombe la Shirikisho wakichuana katika Super Cup na Ahly ambao ni mabingwa wa Ligi ya Mabingwa barani Afrika

Kama ingekuwa bahati kwa Yanga msimu uliopita pengine mchezo huo wangecheza wao kama wangetwaa CAF CC msimu

USM Alger walitwaa CAF CC kwa ushindi wa faida ya bao la ugenini dhidi ya Yanga licha ya timu hizo kutoka sare ya mabao 2-2 katika mechi mbili


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.