Klabu ya USM Alger kutoka Algeria jana ilifanikiwa kutwaa taji la CAF Super Cup baada ya kuichapa Al Ahly bao 1-0 katika mchezo uliopigwa Saudi Arabia
USM Alger ni mabingwa wa kombe la Shirikisho wakichuana katika Super Cup na Ahly ambao ni mabingwa wa Ligi ya Mabingwa barani Afrika
Kama ingekuwa bahati kwa Yanga msimu uliopita pengine mchezo huo wangecheza wao kama wangetwaa CAF CC msimu
USM Alger walitwaa CAF CC kwa ushindi wa faida ya bao la ugenini dhidi ya Yanga licha ya timu hizo kutoka sare ya mabao 2-2 katika mechi mbili



