Simba - Local

CAF CL : Simba uwanjani Zambia

Joel JJ By Joel JJ
β€’
16 Sep 2023
CAF CL : Simba uwanjani Zambia

Wekundu wa Msimbazi Simba Sc leo wanaanza kampeni ya kusaka tiketi ya kutinga makundi katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika

Simba iliyoanzia raundi ya kwanza katika michuano hiyo, leo inachuana na Power Dynamos katika mchezo ambao utapigwa uwanja wa Levy Mwanawasa huko Zambia

Huu ni mchezo muhimu kwa Simba kushinda ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kutinga hatua ya makundi na kuendeleza rekodi yao nzuri katika michuano hiyo

Kwa miaka mitatu mfululizo Simba imeingia hatua ya makundi ya mashindano ya CAF na pia ikifanikiwa kutinga robo fainali

Msimu huu Simba imejiwekea malengo ya kuvuka robo fainali lakini kabla ya kuwaza hatua hizo za juu ni lazima kuvuka hatua za chini kwanza

Kikosi cha kocha Robertinho Oliveira kiko Zambia tangu siku ya Alhamisi jana wachezaji wakipata nafasi ya kufanya mazoezi yao ya mwisho katika uwanja wa Levy Mwanawasa

Jana Robertinho aliwaambia wanahabari kuwa wanatarajia mchezo huo utakuwa mgumu, lakini wamejipanga vyema ili kupata matokeo mazuri

Mchezo utapigwa saa 9 Alasiri kwa saa za Zambia wakati Tanzania itakuwa saa 10 jioni

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
2h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
3h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
3h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
6h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
10h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
11h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
11h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
12h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
12h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
13h ago
READ MORE β†’