Mabingwa wa soka Tanzania Bara Yanga leo wako nchini Rwanda wakikabiliwa na mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Al Merrikh
Mchezo huo wa mkondo wa kwanza kuwania tiketi ya kutunga hatua ya makundi, utapigwa kwenye uwanja wa Pele, Kigali saa 9 Alasiri (saa 10 Tanzania)
Ikisafiri na idadi kubwa ya mashabiki kutoka Tanzania, Yanga leo inaanza mkakati wa kuiondosha Al Merrikh katika michuano hiyo na kutinga hatua ya makundi
Ni takribani miaka 24 Yanga haijacheza hatua ya makundi, kikosi cha Kocha Miguel Gamondi kinasaka rekodi ya kuwarejesha Wananchi katika hatua hiyo baada ya muda mrefu
Msimu uliopita Yanga ilipata mafanikio makubwa katika michuano ya kombe la Shirikisho (CAF CC) ikicheza hatua ya fainali na kuvaa medali ya ushindi wa pili
Msiimu huu Yanga imejiwekea malengo ya kutinga hatua ya makundi, uongozi wa timu hiyo ukiamini kama watafanikisha malengo hayo, watakuwa na nafasi ya kufanya vizuri zaidi katika hatua itakayofuata
Yanga itashuka uwanjani leo kuikabili Al Merrikh ikiwa na kikosi chake kamili
Ni mchezaji mmoja tu, nahodha Bakari Nondo Mwamnyeto ambaye hakusafiri Rwanda kutokana na matatizo ya kifamilia
Baada ya kuanza vyema mechi za hatua ya awali, matarajio ya Wananchi ni kuona timu yao ikiendeleza ubabe katika mchezo huo dhidi ya Al Merrikh



