Yanga yatoa shukrani Rwanda

Joel JJ By Joel JJ β€’ 17th September 2023


Yanga yatoa shukrani Rwanda

Rais wa Yanga SC, Hersi Said ameishukuru nchi ya Rwanda ambayo iliwapokea na kuwahakikishia usalama Wanayanga waliosafiri kwa mamia kushuhudia mchezo wa mkondo wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya wenyeji wao Al Merrikh ya Sudan ambapo Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 2-0

Pamoja na Yanga kuwa ugenini ndani ya ardhi inayoongozwa na Rais Paul Kagame, lakini ni kama ilikuwa nyumbani tu kutokana idadi kubwa ya mashabiki wao kuijaza Kigali na hata mapokezi waliyoyapata kutoka kwa wenyeji wao

Hersi ambaye kabla ya mchezo alimkabidhi Waziri wa Michezo wa Rwanda Aurore Mimosa Munyangaju jezi maalum ya Rais Kagame, amesema Yanga ilikuwa na wakati mzuri Rwanda na inashukuru kwa ukarimu waliopewa

"Tunashukuru kwa mapokezi tuliyopata hapa Rwanda, kwangu ilikuwa heshima kukabidhi jezi ya Yanga kwa Mheshimiwa Waziri wa Michezo wa Rwanda ikiwa ni zawadi maalumu kwa Mheshimiwa Rais Paul Kagame," alisema Hersi

Aidha Hersi amewashukuru Wanachama na Mashabiki wa Yanga waliosafiri kwa wingi Rwanda kwenda kuishangilia timu yao

Hersi amesema wingi wa Wananchi waliosafiri ni ishara ya imani kubwa ambayo Wananchi wameuoa uongozi wake na watahakikisha wanaendelea kuipambania nembo ya klabu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.