Mshambuliaji mpya wa Singida G Elvis Rupia ameifungia timu yake bao pekee la ushindi dhidi ya Future FC ya Misri katika mechi ya raundi ya kwanza Kombe la Shirikisho Afrika
Rupia alifunga bao hilo kwa shuti la mguu wa kushoto akipokea pasi ya kichwa kutoka kwa Morris Chukwu
Rupia alisajiliwa na Singida FG akitokea klabu ya Polisi ya Kenya, akiwa amefanya mazoezi na timu hiyo kwa takribani siku nne
Mfungaji bora huyo wa ligi kuu ya Kenya msimu uliopita ameiongezea makali safu ya ushambuliaji ya Singida FG
Singida itahitaji sare kwenye mchezo wa marudiano utakaopigwa Misri Oktoba Mosi ili kuweza kutinga hatua ya makundi